SITAACHA KUSEMA BLOG HII SI YA MZUNGU WALA MGIRIKI NI MTOTO WA KISWAHILI NA KICHUNA CHA KITANGA.UKIONA UNABOREKA BOFYA KWENGINE.

Friday, October 29, 2010 16 Comments

Siku zote ukweli unauma hata mie mnayonipa na yapata sina roho ya mtutu kila mtu kumlipukia,poleni nawapa na hata mkisema bakora zipo pale pale, binadamu haya ni maneno yangu vipi kama hayakuhusu ikuume? inatakiwa uisome kimya kimya kama plate namba za jeshi mimi umesikia mzungu? sijachanganyika na ujerumani wala uingereza sasa basi nyie mnaotaka kuingia humu inabidi ujizatiti na uswahili huu na hii blog naweza weka chochote hata wewe ukitaka nikuweke,siwezi kumfuraisha jini wakati kiti anakonda kama ALIKUHUSU PIGA KIMYA UKIONA LINAKUHUSU LAKO ILO.Kuna watu wameletwa duniani kuwakera wenzao kwa mie hata hamjanikera bado nawapenda wanaoingia humu na kuupenda uswahili wangu sibadiliki hivi ndivyo nilivyo siwezi kujifanya mzungu ili iweje ukiitaka utabofya usipoweza ipotezee,Na kumbuka raha ya ngo"nda mpike umefunga mlango,na ukiuza utumbo usiogope nzi.

16 comments:

  1. inaelekea kakuchukia kweli dida uyu mtu,jamani we kinyang`unya acha kumchukia mwenzio kiasi hicho,kwani we unakereka nn na dida?nenda kwenye blog nyengine za wazungu hapa kwenye uswahili tuwachie wenyewe.

    ReplyDelete
  2. KAMA VP DIDA MPOTEZEE TU UYO NYANI,

    ReplyDelete
  3. wanafiki hao Dida achana nao! ukiona hivyo wamekukubali, kwani hizo za wazungu hawazioni??? wanafuata nini huku?

    ReplyDelete
  4. Mh kwa tabia hiyo labda ungeolewa na Idd Amin ndo mngewezana, mana ungekua unakula kichapo mpaka mhogo ungeita mhoho....
    Wewe si uswahili tu, ulimbukeni, upumbavu na utaahira kidogo utakua unakunyemelea. Unaharibu maana nzima ya ICT!!!
    Ningekua na uwezo wa kuichakachua hii blog yako kwa virusi, acha tu .... tehe tehe teheeeeeee
    Hayo ni mawazo yangu, si ndo unauza utumbo, usituchoke nzi sie.

    ReplyDelete
  5. Wewe Dida mdogo wangu mamii huwa unanifanya kila siku nifungue humu ndani kuangalia leo umekuja na maneno gani. Yaani huwa nacheka mpaka basi, mbona wanakukoma!

    Halafu kweli kama wao wazungu huku uswahilini wanafuata nini? Eeh bidada waulize vizuri wanakufatia nini uswahilini kwetu? Si wakae huko uzunguni kwao au hakunogi! Kwi kwi kwii! Naomba na mimi unifundishe hayo maneno kweli wewe mtoto wa Tanga na Kimanyema maana mdomo unao hasa. Mimi naomba uniruhusu nitumie huo msemo wako wa "siwezi kumfurahisha jini wakati kiti anakonda!" Hehehee halo ya leo kali umenifanya mpaka nimepaliwa na chakula!

    ReplyDelete
  6. Mimi nashangaa sana mashauzi ya kizungu kuna watu wanayazimia kweli, kuna blog watu wanajisifia kiiila siku na picha nyingine wala hazitusaidii maishani ndio mnaona ustaarabu? Dida mtoto wa pwani na blog yake ya kipwani mwacheni ajidai kwenye uwanja wake. Ni mswahili na yuko proud sasa nyie waswahili mnaoutukuza uzungu msiingie humu ndani kabisaa tuachieni kauzu zetu na nyanya chungu na nguru tujisonsomole

    ReplyDelete
  7. siku zote hata kama mtu kasema maneno yamekuumiza usipende kumuonyesha kwamba limekupata kwa kumjibu mkalie kimya mwisho wa siku atajiona mjinga nae atanyamaza lakini kujibu kwako unapalilia hali ya majungu kuendelae usipende adui akujue uko upande gani ili uweze kumshinda dida kazi njema

    ReplyDelete
  8. duu kumbe mtoto wa kitanga basi hapo starehe tupu

    ReplyDelete
  9. hahah dida umenifurahisha na misemo yako hata sijui ngonda maana yake nini jamani wadau hebu msaada wengine sie watu wa bara hatujui ngonda ukimpika ufunike hahaha yani sielewi nikitu gani

    swahiba

    ReplyDelete
  10. Duu! Kweli wewe hushauriki! Wengine hukushauri kwa nia njema kabisa. Kwa vile leo umesema hutabadilika basi kuanzia leo na mimi ntakuwa NZI maana umeamua kuuza utumbo! Ha ha ahaaaaaaaaaaaaaaa! Mbavu zangu mie!lol!

    ReplyDelete
  11. Jamani tujuzeni wengine basi! Ni kina nani hao wazungu wanaomsumbua Dida?!!???!

    ReplyDelete
  12. Dada wa bara ng' onda ni samaki mkavu aliyeanza kama kuoza hivi au wakati mwingine anakua hata hajaoza, anapakwa chumvi kibao na kukaushwa kwa jua. Sasa hiyo harufu yake usiseme ni ya uvundo ukimbeba kila mtu anajua umebeba ng'onda ila mtamu kwa nyanya chungu na bamia kisha umtie nazi, kipande kidogo waweza maliza sufuria ya ugali. Akichomwa mpaka mtaa wa pili watajua kunachomwa ng'onda leo!

    ReplyDelete
  13. humu umbea hakuna sijui kusema K alimsema Q kwamba M katembea na Z mambo hayo ya ushankunaku humu hakuna kabisa, ni mipasho lenye kumchoma limchome lenye kumvutia limvutie lenye kumuudhi akanywe maji akalale. Kama ni nzi wazidi kufuata utumbo maana mavi na harufu wanavipenda mpaka wafie utumboni au sio Dida? ndio maana yake!

    ReplyDelete
  14. mama hatusemei uzungu wa ukabila tunasemea tabia yako shostitooooo.kama waleeeeeeeeeeee .hahahahha poleee mwayaaaaa

    ReplyDelete
  15. Shost hakuna cha wazungu wala nini! Ni yeye tu akishauriwa apunguze uswahili (maneno ya vijembe yasiyo na maana yoyote) anadai wanaomshauri hivyo wanajifanya wazungu.

    ReplyDelete
  16. mi naomba nikushauri kitu kimoja,punguza podaaa mama,unaipaka kupitiliza mpaka inaboa badala yakupendeza unatisha.

    ReplyDelete