WAPENZI WA SOKA KUMUAGA MAREHEMU MAFISANGO LEADERS KESHO ASUBUHI

Thursday, May 17, 2012 0 Comments


 MWILI wa  aliyekuwa kiungo mkabaji wa Simba ya Jijini Dar es Salaam, Patrick Mutesa Mafisango, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo kwa ajali ya gari maeneo ya Tazara, Dar es Salaam unatarajiwa kuagwa kesho saa 2 asubuhi katika viwanja vya Leaders Club, Kinondoni. 

Meneja wa Simba SC, Nicodemus Nyagawa amesema kuwa, baada ya zoezi la kuagwa mwili huo,  utasafirishwa kwa ndege ya Shirika la ndege ya Kenya,KQ kuelekea nchini Kigali Rwanda kwa shughuli za mazishi. 

Wapenzi wa Simba na Mashabiki wa Soka wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuaga mwili wa marehemu Mafisango, aliyekuwa kiungo tegemeo wa klabu hiyo katika msimu wake mmoja wa kuichezea tangu ajiunge akitokea Azam FC.

Akielezea chanzo cha ajali hiyo, Nyagawa alisema kuwa kwa mujibu wa taarifa alizopata ni kwamba, Mafisango aliyekuwa akiendesha gari lake mwenyewe, alikuwa akijaribu kumkwepa dereva wa pikipiki na kwa bahati mbaya akaingia mtaroni na kuumia kabla ya kufariki dunia.

0 comments: