NAOMBA NIWATENGUE UDHU KIDOGO WADAU,KUOLEWA NA KUACHIKA NI JAMBO LA KAWAIDA KAAACHIKA MAMA WINNIE MANDELA NA DUNIA NZIMA IKAJUA,SEMBUSE WENGINE.

Tuesday, April 19, 2011 25 Comments

UNJUA NAOMBA NIANDIKE KWA HERUFI KUBWA MLIOKUWA HAMUONI MSIUMIE MACHO,WAPO WENGI TULIBAHATIKA KUOLEWA NA SIKWAMBA WAZURI SANA ILA NI MIPANGO YA MWENYEZI MUNGU SASA NIWAHABARISHE NYIE AMBAO KILA KUKICHA KUWAAMBIA WENZENU NDIO MAANA MMEACHWA WENGINE TUMEACHA SI LZM UTANGAZIWE NA HATA TALAKA HATUJAPEWA KUACHWA SI TIJA KWANI HUJAZALIWA NAE,SIJUI NYIE MNAOFANYIWA VISA MNASHINDWA KUTOKA KWENYE NDOA ZENU ETI MNAOGOPA KUONEKANA MMEACHWA KWA MANENO YA MAVUVUZELA WASIO NA KAZI POLENI MANENO HAYAMBABUI MTU,LABDA KAMA KWENU WALISEMA AFADHALI UMEOLEWA,HATUJAUWA MAKWETU NA WALA HATUWEZI KUZIWEKA ROHO ZETU JUU KAMA FENI MBOVU,HAPO MLIPO NYIE MNAOWASEMA WENZENU KILA SIKU WAMEACHWA WEWE USHAWAHI KUCHUMBIWA AU BADO UNAZEEKEA KWENU AU UPO KWENYE FOLENI KAMA KWA BABU LOLIONDO?TUNAWAITA WASUBIRI MANUSURA ACHENI HIZO WAMEACHWA WATU KIBAO MASHUGHULI WANAJULIKANA DUNIA NZIMA SEMBUSE SISI VITONGOJINI,MMEWAKAA WENZENU KAMA VIDAKA TONGE UKIJUA KUOLEWA JUA NA KUACHWA NA UKIJUA KUTONGOZWA JUA KUKATALIWA NI HAYO UKISIKIA YALAAAA LAKO ILO.

25 comments:

  1. DIDA WAPE NA HATA WAKIONGEA KUACHWA SUNA BIBI SI WAJUE KUINGIA ULIPOINGILIA NDIO UTAKAPO TOKEA WANAJUA WAMEFIKA

    ReplyDelete
  2. KWI KWI KWI mama mbavu zangu ....( foleni ya kuolewa km kwa babu huh!)wamekushika pabaya eh...
    hapo mi nasema tenaaa!kweli kabisa kuna watu wamekalia tuu kusema wenzao mpaka mtu unakua mnyonge jamani, mateso ya kwny ndoa + ya kuachika na kulea watoto mwenyewe+ kusemwa na kunyooshewa vidole na waja jamani mtu weza kufa ghafla kama huna roho ngumu.. dida wape za uso kabisaa watu wenye tabia hii,im behind u 100%

    ReplyDelete
  3. Hilo nalo neno Dida! Unajua wanawake wengine sijui wako vipi, eti anakaa kwenye ndoa isiyo na amani, mwanaume ana mnyanyasa, ana mcheat, anampiga, eti bado yupo, ukiuliza eti ohh watu watanionaje? Hivi ndugu umeolewa kwaajili ya watu au ilikuwa uamuzi wako? Kama ni uamuzi wako basi ukiuona maji yamezidi unga koroga uji bibi! Mwanaume akianza huwa haachi! Hata akiomba msamaha eti ohh ni leo tu niwie radhi, trust me atarudia! Kucheat kuko so addictive kama addiction nyingine! Wanawake tujikomboe, tuwe wasomi, wajasiriamali, tujiajiri, tuajirwe, ili tuheshimiwe. Wanaume wengi huwa wana visa pale wanapojua mwanamke anamtegemea kwa kila kitu, so anafanya mambo yake kwakuwa anajua huyu goli kipa ataenda wapi? Nami namlisha na kumvisha! Wanawake tukomboke! Mie niko nje kwa sasa, huku watu hawataki masihara, kuna hadi ndoa za mkataba, mambo yakicheua kila mtu na lwake! Women we should learn to stand on our own and move on!!!

    ReplyDelete
  4. haloooooooooooooooooo haloooooooooooooo sema mtoto wa kike, sema mama Dida nakupenda japo sikufahamu, mie niko u.k nimependa mawazo ya dada hapo juu April 20...18:28...

    laiti hao wanaosema kuolewa kuachwa wangejua kuwa sio deal wangetumia muda huo kutunga nyimbo kama Jay Dee, ili wapate pesa za kuwafanya waishi, maana sauti wanazo za kuongelea , ahahahahah, aloooo, ushamba tu au elimu ndogo ndio inaweza kukufanya kuongelea kuolewa kuachwa, kunya mavi, watu tuliolewa na watu wako bank of Tanzania na tumewaacha waume na kuangalia maisha salama, ufe kisa nimeolewa!!! itakula kwako mama, wanawake acheni ulimbukeni wa mawazo, mkue, mwaka 2002 sio 2011...fanya kazi, tafuta raha ya moyo wako, angalia wanao kama unao, songa mbele......wanaosema jua ufahamu 10% kichwani.....

    ReplyDelete
  5. Asikudanganye mtu Dida rizki huombwa hailazimishwi ukiona sehemu hakieleweki ujue imekwisha hiyo omba upate kwengine sisemi wanawake wwe wanahamahama km ndege laa hasha ila inawezekana pale ulipo mungu alisha funga mlango kaufungua pengine je utapataje bila wewe kutoka? Twalaka nyingine dawaa wangapi walikuwa kwenye ndoa hovyo na wakatoka mambo swafii kuachwa hata m'mungu karidhia japo hapendi sijui wenzetu wanachukuliaje neno kuachwa kwani mpo jela kifungo cha maisha? basi kuna msamaha wa Rais

    ReplyDelete
  6. dada yng hapo juu swadakta inahusu ufe kiofisa na tai shingoni!!?? ukiona nguo inabana shart kuivua ,eti watu wanaogopa kuachika watoto ntawapeleka wapi ukiwa unafanya kazi au biashara au kuingiza kipato hata mume hatakufanyai ujinga ila tukiwa magoli kipa yatatufika makubwa wanawake hakuna kulala twende nao sako kwa bako wakimwaga mchuzi tunakula mkavu halali mtu njaa hapa karne nyingine hii.
    Sauda Mkalok

    ReplyDelete
  7. lakini wew Dida me nakushangaa sana. niliwahi kukusikia mwenyewe kwamasikio yangu wakati bado umeolewa na Mchops kwamba hautamwacha hata ukimfumania! sasa tena ilikuwaje shostito? mana wakati wamapenzi mtu unajikuta tu unaropoka bila mpango. by the way vipi ndoa yako na muimba taarabu maarufu bongo, mzee Yusufu?

    ReplyDelete
  8. Safiii Dida nimeipenda hiyo, na mwanamke lazima ujiamnini sio unaogopa kuachwa eti ooh watoto wataishije, bibi wee kama una kazi yako kwanini uogope kuachwa kwani ye alikuwa anakupa kitu gani cha zaidi cha kukufanya wewe ushndwe kuishin... mwanaume akileta nyodo tupa kule angalia ustaarabu mwengine.......

    ReplyDelete
  9. naomba usiibane coz inakutachi, hivi huo ushauri wa kikahaba mnaupataga wapi? hayo yote ni maneno ya mkosaji ndoa zimewashinda mnajifanya ooh tuwe tunajiamini oooh mara wajasiriamali kwani hamkugundua kabla hamjaolewa any way dida nafahamu kama unamatatizi kwani sifikirii kama unaweza kuwa na mawazo ya maana mfano niliuona ulipogoma kupiga nyimbo za 5star kisa hukutajwa kumbe ulijifanya unamajonzi tukajua kweli ila ulikuwa unatafuta umaarufu wa kuwepo kwenye orodha ya shukurani utajibeba.

    itoe usiibanie maana unapenda kusifiwa tu

    ReplyDelete
  10. Yani mm nimefurahishwa sana na comment ya pili kutoka mwanzo 20/04/11. Yani nikweli kabisa. Ila niujinga tu wawatu wenye upungufu wa wakili na uwelewa wa kutosha. Kila likuepukalo huwa lina kheri na ww. Ukiona ndoa haielekei mapema jiachie alafu utaona milingo mingine inavyofunguka. Tena bila hata ya kujali kuwa watoto watakula nn wala wala utaishije. Namambo yataenda sawa na utashangaa, Ulikuwea wapi siku zote.

    ReplyDelete
  11. nina sijawahi hata changia ilo nalo nalo neno lakini maneno yako yanikosha kweli wengine wananyanyasika kwenye ndoa kama kwenu uliuzwa ukaambiwa usirudi , mie nilivyoelewa kwenye send off my dad alisema atujakuuza nafasi yako bado iko home tu hahhahhahahahh

    mdau canada

    ReplyDelete
  12. Sema Dida wape vidonge vyao hayo manungaembe, wengine ndoa zao chungu wanalia kila kukicha lakini bado wanang'ang'ania eti aonekane naye yuko kwenye ndoa. Mie nimeacha na niko majuu maisha yangu yamenyoka mpaka nasema nilichelewa wapi. Kila jambo lina sababu zake linapotokea. Asikurushe mtu roho my dear.

    ReplyDelete
  13. Dada yngu uliye comment tarhe 22, time 8:18am usiwe mbinafsi hebu hurumia wanawake wenzako, inamaana toka umejua ndoa ninini mpaka hapo ulipofikia hujawaona wanawake wenye jehanam ya dunia katika ndoa na hujawahurumia? kama haujaona basi sina sababu ya kukulaumu ila inshallah kama si wewe basi hata mwanao yatamkuta, nitakuona wa ajabu sana ukivumilia au ukimshauri mwanao avumilie ndoa kwa karne hii tuliyonayo we wa wapi? ndoa za sasa zina kila aina ya balaa kama haukoswa na uchawi basi utakumbana magonjwa au hata utatumiwa watu wakudhuru nina ushahidi wa haya nisemayo baada ya mwanamke kujifanya kichwa ngumu kuvumilia kuliko kuepusha roho yake, "tembo hashindwi na mkonga wake" hakuna iliyomshinda ndoa ila narudia karne hii si ile ya enzi za mwalimu kuvumiliana mateso kama walivyofundwa bibi zetu, nafsi huvumilia dhiki kwani kupata majaaliwa lakini si maudhi dada yanachosha kwani mwenzetu huna kwenu?

    ReplyDelete
  14. kweli kabisa Dida wape hao wamezoea!!!! Unajua wanawake kibao anakaa kwenye ndoa isiyo na amani, mwanaume ana mnyanyasa, ana mcheat, anampiga, eti bado yupo, ukiuliza eti ohh watu watanionaje? Hivi ndugu umeolewa kwaajili ya watu au ilikuwa uamuzi wako. Mi pia nakusupport 100% mammy ma namimi ni kama wewe tu na MAISHA YANAENDELEA KWA RAHA ZETU.

    ReplyDelete
  15. nimeipenda hiyo sn tu! wanaume wanamanyanyaso sn.

    ReplyDelete
  16. mmhh! hiyo kali ati

    ReplyDelete
  17. mmh hapo d umegusa wengi maana tunavyozibeba hizi ndoa kwa nguvu zote utatadhani tulizaliwa nazo ndio maisha lakini wanaume wa kibongo wamezidi sijui wenzetu majuu.

    ReplyDelete
  18. wote mmekutupuka ndoa inamashart na nguzo zake nyie mliolewa ili mfanyiwe k party tu hakuna alie na sababu ya msingi kwenye ndoa ukifata mashartna nguzo zake utakua pamoja na mmungu wadada wa mjini mnapenda mapenzi mapya kila siku hamna subira wala imani mnataka kila siku take away amkai mkapika jikoni

    ReplyDelete
  19. Saf hiyo kweli dida umeongea dada yangu,wanaume wana mateso sana na wanawake tulivyo wajinga tunawaendekeza kwa kuwavumilia tu utadhani umezaliwa nae..tujifunze jamani hata wao wakiona tuna misimamo watakosa wa kuwanyanyasa watatulia tu...Go galll achana na maneno ya watu,kama yamewazidi waandike nyimbo waimbe, Ila kweli wanaweka wenye misimamo ni wale wasiovumilia ujinga eti kisa wameolewa wanaogopa kusemwa vibaya...

    ReplyDelete
  20. Baada ya beijing wanawake wengi wamekuwa na midomo midomo ndio maana ndoa nyingi hazina amani, Mwanamke aliyelelewa vema nyumbani kwao ni aghalabu kuachika, wale wanaoachika ujue wamedekezwa sana huko nyumbani kwao walikolelewa....muwe waangalifu!

    ReplyDelete
  21. Mtu unaolewa ili ukawe mpishi au mashine ya mume ya kufulia nguo? Hivi nyie mnaosema kuwa eti mtu hapiki pengine mnaongelea noa za imani nyingine lakini imani ya kiislam kazi ya mke ni moja tu na wajibu wake umeanishwa wazi kwenye Quran na Sunna za Mtume SAW. Na mume kama ana uwezo anapaswa aweke watu wa kufanya hizo shughuli. Kwenye uislam hata kunyonyesha mtoto mume inampasa amlipe mkewe ikiwa atamsamehe basi ni sawa. Na mengineyo yote atakayoyafanya kama kupika, kufua, na kufanya usafi anafanya ili apate malipo kutoka kwa mola wake na anajitolea. Sasa nyie mnaosema mke kazi yake kupika basi hao waume wangeweka machefs kwenye nyumba zao ili wapikiwe lakini upishi wa mke sio jikoni mapishi yake ni kumpa UTULIVU mume wake! Apate utulivu wa nafsi apate chakula cha nafsi! Basi!

    ReplyDelete
  22. Hebu wape elmu hao shosti uliyecoment hapo juu, watumwa wa mapenzi hao eti hatukufundwa sijui hatupiki, eti k-pat, sijui na nini, ivi we unayejifanya unajua nguzo za ndoa unayajua hayo km wewe ni tunda la kuwekwa ndani tu ukasubiri kazi moja, ebu tafuta elmu kwanza alafu angalia lipi analotimiza mumeo ndio utaona haki yako inatimizwa au we ni mtumwa tu kwa mumeo, mwenyezi mungu ameridhia ama kamuamuru mume kutoa twalaka kwa mke ikiwa hawezi kutimiza masharti ya ndoa ikiwa we unamvumilia nina hakika si kwa mapenzi bali ndio walewale "ntachekwa nikiachwa" unaibeba dhima bidada

    ReplyDelete
  23. watajibeba na ndoa zao za jehanamu hao wanaoona ndoa ni mchongo sana.

    ReplyDelete
  24. we dada wewe uliecomment April 22 8:18, Mungu hapendi kuwaobea mabaya wanadamu wengine lakini mie nakuombea wewe Mungu akupe ndoa kama niliokuwa nayo mie... ukivumilia wewe ni sugu umeua kwenu huwezi kurudi... yani umenitia uchungu sana Mungu akushuhsie mwiba wa ndoa. sina kingine

    ReplyDelete
  25. wape hao Dida vidonge vyao mi nakuunga mkono na miguu kwa raha zetuuuu mamitoooo kuolewa na kuachwa ni jambo la kawaida.

    ReplyDelete