HUWA NA FARIJIKA SANA IKIFIKA WEEK END NAPENDA KUKAA KARIBU NA SAMIRA WANGU KUJUA ANAPENDA NINI.

Saturday, February 05, 2011 24 Comments

Ni raha sana duniani kupata mtoto anayekupa faraja maishani,Ikifika week end nasikia raha kukaona kabinti haka mtalala ikifika asubuhi katakuacha kitandani utakaita mpaka koo likukauke ukitaka kujua yuko wapi mhhhhh.
Unakakuta kamejilaza kanaangalia movie nahisi anazimic tu kwa ajili ya shule huwa najaribu kumchungulia hasa movie gani anaipenda ni MY DREAMS ukimuuliza anakwambia nampenda RAY NA IRENE ok,Ni kubadilisha mikao mara kakukunjia nne chezea yeye.
Yaani unamtoaje?
Kilichonifanya nikacheka zaidi kaona kama akilala haoni vizuri kaenda kuvaa na hayo manyoya labda ataona vizuri huwa nafurahi sana.
Akimuona huyo mwanadada anafurahi mbaya mungu endelea kunikuzia kiumbe huyu ishallah ananipa raha maishani walahiii.

24 comments:

  1. Nami nimemfurahia sana mrembo huyo. Mshushie kidogo hiyo TV mi naona kama anaumia shingo kutizama juu kwa muda mrefu. Msalimie sana.

    ReplyDelete
  2. Amina tunakuombea Allah amkuze binti huyu, amuepushe na yote mabaya, amuweke mbali na husda,fitna za walimwengu, awe mtoto mwema mwenye mapenzi ya kweli kwa mama yake na nduguze, amjalie elimu dunia na elimu akhera, sema amina

    ReplyDelete
  3. hongera dida,pia mungu atampa uhai mrefu inshaalah,

    ReplyDelete
  4. m mngu aakutunzie mwanao inshaallah awe mtoto mwema mwenye mapenzi na kila mtu isipokuwa ilee midume mishenzi

    akuheshimu atuheshimu na awe mtoto mwenye ufahamu mzuri shuleni halooooo jicho la husda lisimpateeeeee

    shosti pale kwenye hiyo mizizi maua juu yake tafuta frem mooja hivi inayo match na carpet may be green na hiyo red sijui ama red pink then wek ahapo juuu yani itafungua sitting room hado raha by the way mwanawane wajua kupambaaaaa nimepeenda sio mavitambaaa na maua nyumba nzima hahahaha

    kishuuuna

    ReplyDelete
  5. Amin ishallah ahsanteni wadau nashukuru na mdau kwa ushauri wako mzuri nitaufanyia kazi nitapiga tena ili unishauri kama nimepatia si yote tunayajua ila ukipata mtu akaakuelekeza inakuwa vizuri ahsanteni sanaa.

    ReplyDelete
  6. No offense hizo movie za kina Ray kwa watoto hapana kwa kweli,watoto wangu ni wakubwa kuliko wa kwako wala siwaruhusu kuangalia. Labda zinazo husu watoto kana uncle JJ na nyingine. Otherwise nyumba ni nzuri na umeipamba vizuri

    ReplyDelete
  7. ahsante kwa ushauri mamii nitautekeleza nitamuwekea kina auncle jj nashukuru sana

    ReplyDelete
  8. Hongela nyumba umeipamba vizuri ipo simple sana na imependeza kikweli. ila nasisitiza mtoto kwa movie za bongo si nzuri kwa yeye kwani wao hawachagui mavazi wala maadili yetu wameyasahau. mpatie za katuni ni nzuri zaidi kwake

    ReplyDelete
  9. Binti yako mzuri sana mungu akukuzie shosti nyumba yako nimeipenda hongera.

    ReplyDelete
  10. nimeipenda nyumba mwaya......yaani simple lkn yavutia kweli, Mungu amjalie maisha marefu mwanao awe na akili sana hata darasani.....usipende kumwekea movie hizo hazina maadili sana labda zile za uncle jj au cartoons atleast. gud day hi kwa ur baby gal

    ReplyDelete
  11. uwiiiiiii hizo si nzuri kabisa kwake, hawa watoto wanaakili kushinda watu wazima yaani wanacatch mambo kwa haraka sana, kuna movies nyingi sana za watoto mtafutie atazipenda tuu but hongera mwanao ni mzuri na mwenye afya

    ReplyDelete
  12. tv iko juu sana haoni vizuri mummie ishushe kidogo, mwanao mzuri ile mbaya

    ReplyDelete
  13. Hongera dear mtoto mzuri sana Mungu atakukuzia tu.Nakushauri tu usikubali mtoto aangalie hizo movie za watu wazima, jitahidi uwe unamwekee cartoon zitamjenga akili zaidi. Kwa sisi tuliokuwa nje ya nchi ni kosa kubwa sana mtoto akikutwa anaangalia movie za watu wazima.

    ReplyDelete
  14. Cute gal, Mtyotyo yuko bomba, naomba niwe baba mlezi,
    mduduvule@yahoo.com

    ReplyDelete
  15. mduduvule umenifanya nichekee siku ya leo.

    ReplyDelete
  16. dida nilikuomba upost clip za vipindi vyako kwenye blog yako wengine hatupo nyumbani tz ila umenichunia tafadhali dadangu tupostie na sie tusikilize

    ReplyDelete
  17. duuu wewe demu mtafutaji sana potelea mbali wakuseme hapo umewaonyesha nusu je wangeona upanda wa pili chezea lzm wakuchukie si wote unajitahidi na maisha yako wanga wanaumia kama mdau wa blog hii tupigie na upande wa pili wajute kufungua midomo yao safi sanaaaaa mungu akukuzie mwanao dida

    ReplyDelete
  18. NDIYO MAANA ANAWACHAMBA KUMUITA MASHAUZI INAWAUMA NA MAISHA YAKE NYOOOO.

    ReplyDelete
  19. Sawa mamii uliyeomba niweke clip za kipindi nitafanya hivyo nathamini maombi yako

    ReplyDelete
  20. Dida mi ni mzazi na nina imani una dstv wana cartoon network ambayo mtoto anapata karibu cahnnel 5 za cartoon mi wangu anajua cartoon zote halafu unajua cartoon zinafunza mtoto anajua lugha na mambo mengine ya kieleimu, mtoto anapata ufahamu mahsusi kwa watoto achana na hizo uncle jj wala bloody kanaumba, mwache mtoto awe mtoto.

    ReplyDelete
  21. hata uncle jj sio nzuri,wewe ulisikia pale jenifer anamuita uncle wake 'BI MDOGO' SIJUITUKAOLEWE WOTE what the heck halafu baraza letu la sanaa na utamaduni liko kweli?mpe mtoto katuni hizo za kina kanumba hazina maadili zinatufaa sie watu wazima sio watoto wetu.

    ReplyDelete
  22. dida nyumba yako nzuri piga picha nyumba nzima tuone unapolala na jikoni kwako na mimi naongezea tv iko mbali sana na mtoto anaumia shingo mwekee katuni za watoto mwanao bado mdogo kwa hizo movie hazimfai otherwise unafanya vizuri

    ReplyDelete
  23. Nnachokupendea we dada ni mtafutaji hasa, nakumbuka sana ulipotokea kipindi kile ni muigizaji mpaka ulipofikia sasa kwa KWELI nakukubali, na Unanigusa sana kila ninapoona maendeleo yako Mungu aendelee kukujaalia, Ila mashauzi punguza

    ReplyDelete