FAMILIA YA LADY JAY DEE WALIPOTEMBELEA KITUO CHA WATOTO YATIMA CHA MAUNGA - KINONDONI

Tuesday, July 03, 2012 0 Comments

Lady Jay Dee akipokea risala kutoka kwa mtoto Khadija Mussa.
Lady Jay Dee akikabidhi msaada uliotolewa na Familia yake vikiwemo Mchele, Maharage, Mafuta ya Kupikia, Sabuni za Kufulia, Nguo, Juisi pamoja na vingine vingi. Anayepokea msaada huo ni Mlezi wa Kituo hicho  Bi. Zainabu Bakari (kushoto) pamoja na mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo hicho Khadija Mussa.
Jay Dee Family inawakaribisha wadau wote watakaoguswa kutoa mchango chcochote walichonacho kupitia Jay Dee Family. Kwa mawasiliano zaidi wasiliana na Judyjaydee@yahoo.com.

RISALA FUPI KWA MGENI RASMI - KUTOKA MAUNGA CENTRE

Ndugu Mgeni Rasmi

Maunga Centre ni kituo cha kulelea watoto yatima na waishio katika mazingira magumu.
Kituo kimeanzishwa mwaka 2008 na kusajiliwa mwaka 2011
Kituo kina watoto 50, kati yao 30 wanaishi hapa kituoni na 20 wanaishi na walezi wao.
Lakini mahitaji ya kibinadamu wanayoyapata hapa kituoni, Sisi kama viongozi wa Maunga Centre hatupendi watoto hawa kuishi na walezi wao, ikizingatia kuwa hawana uwezo ila kutokana na uchache wa Vyumba imelazimika iwe hivyo.
Uongozi wa Maunga Centre unatoa shukrani za dhati kwa kukubali wito wetu wa kuja kuwatembelea na hii inaonyesha jinsi gani unavyopenda jamii bila ubaguzi.
Maunga Centre ilituma barua kwako ya maombi ya kuwatembelea watoto hawa yatima ambao hawakupenda kukosa wazazi wao. Tulituma maombi kwako kwasababu tuna imani kubwa kuwa wewe ni kioo cha jamii na mpenda jamii bila ubaguzi wa rangi, dini, jinsia, wala ukabila wewe ni mtu wa watu wote.
Kitendo ambacho leo umekifanya cha kuwatembelea watoto na kula nao chakula pamoja ni kitendo cha kihistoria kwa jamii ya Watanzania na tunaamini umefuata maagizo ya Mungu kwa dini zote.
Tukumbuke kuwa tendo la kuwatembelea yatima, kuwasaidia, kuwafariji kwa kuondokewa na wazazi wao ni ibada au sala kubwa sana kwa Mungu
Tunawashukuru wote ambao umeungana nao katika msafara wako sisi kama kituo tunasema hatuna cha kuwalipa ila malipo mtayapata kwa Mungu, pia tunawaombea Mungu awape uzima, kipato na awapandishe vyeo uko kazini kwenu ili kipato kiongezeke muweze kusaidia jamii hususani yatima.
Maunga Centre inatoa shukrani kwa misaada ambayo mmetuletea. Kituo cha Maunga Centre kinawaomba MR.&MRD GARDNER kuwa walezi wa kituo hiki,
Tunawaomba kuwa walezi kwakuwa tunaamini kitendo ambacho leo mmekifanya inaonyesha jinsi gani mlivyokuwa na uchungu na swala zima la yatima.
Tunaamini kuwa kutoa ni moyo na wala si utajiri kwasababu wapo wenye uwezo mkubwa lakini hawajitoi kusaidia jamii kama ulivyofanya leo.
MAUNGA CENTRE ina changamoto zifuatazo:
1. Kukosa fedha za kuwalipa wahudumu
2. Kukosa eneo kubwa la kujenga kituo
3. Kukosa wafadhili
4. Watoto hawana sare za shule
5. Kukosa gharama za kuwasomesha (michango ya shule)
Tafadhali tunakuomba ututafutie wafadhili wa ndani na nje ya nchi ili tuwasaidie na tuna imani kubwa kuwa unawafahamu watu ambao wana moyo wa kutusaidia wa ndani na nje ya nchi.
Tunakuomba utusaidie kukitangaza kituo katika vyombo vya habari ili watu wenye moyo watusaidie.
Sisi kama kituo hatuna uwezo wa fedha za kugharamia gharama za matangazo.
Ndugu mgeni rasmi tunakuomba tamasha moja la muziki la kuchangia fedha kwaajili ya kituo cha watoto yatima. Tunakuomba malipo utayapata kwa Mungu.
Mwisho tunakutakia maisha mema, Mungu akupe roho ya imani pamoja na kipato kiongezeke zaidi akupe kizazi chema ambacho kitajali jamii kama ulivyo wewe mwenyewe
Ahsante
Karibu tena Maunga Centre
BINAFSI NINGEPENDA KUANZA NA KUWATAFUTIA KIWANJA KIKUBWA KWAAJILI YA KUJENGA  KITUO KINGINE. WAHAME HAPO WALIPO, WANABANANA SANA NA NI VYMBA VIWILI TU AMBAVYO VINA HALI MBAYA SANA.
AKITOKEA MTU WA KUTUSAIDIA KIWANJA, TUTACHANGISHA FEDHA ZA KUANZA UJENZI:

Mimi kama JAYDEE natoa wito kwa yoyote mwenye moyo kuungana nami katika swala hili.
Ikiwa mimi na Gardner tumeombwa kuwa walezi wa kituo hicho, Pamoja tunaweza

Natanguliza shukrani:
JIDE 
 Hivi ndio vitanda wanavyolalia watoto hao.
Watoto wako 30 na vyumba viko 2
Sasa fikiria ni wastani wa watoto 15 katika kila chumba

Hakuna mtu yoyote ambae angependa kuishi katika mazingira ya namna hii, huruma ndio inayohitajika hapa
 Hili ndio eneo wanalotumia kama jiko la kupikia chakula

Na hii ndio sehemu ya kujisaidia "CHOO"
Fungua moyo wako, tafadhali i beg you pipo
Haya sio maisha watoto wetu wanayostahili kukulia
Tusaidiane kujikwamua katika umasikini ili hata wakienda shule waweze kufikiria masomo na kufanya vema
Msafara ulianzia Nyumbani Lounge ambapo LA FAMILLE tulikutana na kila mmoja alileta kidogo alichonacho ili kuchangia watoto wa kituo cha MAUNGA

Sehemu wanayoishi watoto hao wenye ni sehemu ambayo mazingira yake sio ya kuridhsha kabisa
Kwa mtu yoyote akifika hatasita kutokwa na machozi
Hii ni njia ya uchochoro ambayo inaelekea kituoni hapo
Gari haiwezi kupita hivyo ilitulazimu kupaki barabarani na kutembea kuelekea kituoni, kama inavyoonekana kwenye picha
Huyu mama ndio mlezi wa kituo hicho
Pamoja na hali duni iliopo kituo hicho walijitahidi kupamba na kutuandalia mazingira tujisikie kama wageni


Watoto wengi ni wenye umri mdogo sana ambao wanahitaji malezi na uangalizi wa hali ya juu


 Beautifull
 GK akisaidia kushusha vyakula vya msaada kituoni hapo

 Nyumba wanamolala watoto hali yake si nzuri hata kidogo

 Vitanda ni vichache kwahiyo huwalazimu kubanana

 Happy Happy

 Wanty
 Maggie Musa na Leon Lee

 Sab

 Wise Monica Kaaya

 Tulijikuna mpaka hapa japo kuna mengi wanayoyahitaji zaidi




 Faraji


Binti alisoma risala ilioelezea matatizo wanayokumbana nayo kituoni hapo
Sisi kama LA FAMILLE hatukwenda kituoni hapo kwaajili ya show off bali waliniandikia barua ya kuomba msaada nami nikaona ni vema kusaidiana na wenzangu.
Na wanahitaji kutangaziwa zaidi ili watu wengi wajitokeze kusaidia kwani hali yao ni tete ki fedha na kimahitaji


Nili play part yangu mpaka hapa ila kwa bahati mbaya nasikitika kuwa sikuweza kukaa muda mrefu na kula chakula cha mchana pamoja na watoto hao kutokana na kuwa ilinibidi niwahi airport kuelekea BUNDA kwa mazishi ya bibi yangu.
Ila mimi pamoja na staff wa NYUMBANI LOUNGE tuliandaa chakula na niliacha LA FAMILLE waniwakilishe kwa ratiba iliobakia
PICHA ZOTE NA MAELEZO YANAYOFUATA KUANZIA HAPA NI KWA HISANI YA ZAINUL MZIGE WA MO DEWJI BLOG
Lady Jay Dee na baadhi ya wanafamilia wakipiga makofi baada ya risala kusomwa na mtoto Khadija Mussa (hayupo pichani).
Lady Jay Dee akipokea risala kutoka kwa mtoto Khadija Mussa.
Lady Jay Dee akikabidhi msaada uliotolewa na Familia yake vikiwemo Mchele, Maharage, Mafuta ya Kupikia, Sabuni za Kufulia, Nguo, Juisi pamoja na vingine vingi. Anayepokea msaada huo ni Mlezi wa Kituo hicho  Bi. Zainabu Bakari (kushoto) pamoja na mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo hicho Khadija Mussa.
Jay Dee Family inawakaribisha wadau wote watakaoguswa kutoa mchango chcochote walichonacho kupitia Jay Dee Family. Kwa mawasiliano zaidi wasiliana na Judyjaydee@yahoo.com.
Lady Jay Dee akibadilishana mawazo na walezi wa kituo hicho baada ya kukabidhi msaaada huo.
Mwanafamilia Ester Ulaya (kushoto) akiteta jambo na Komando Binti Machozi Lady Jay Dee.
Pichani Juu na Chini Wanafamilia wa Lady Jay Dee wakipakua chakula kilichoandaliwa Nyumbani Lounge kwa ajili ya kula pamoja na watoto yatima wa kituo cha Maunga Centre.
Watoto wa kituo cha Maunga Centre wakipata chakula cha mchana kilichoandaliwa na Jay Dee Family.
Vijana wa Jay Dee Family wakiwajibika kuhudumia chakula kwa kituo cha kulelea watoto yatima cha Maunga Centre.
Mlezi wa kituo cha Maunga Centre Bi Zainabu  Bakari ambapo amezungumzia changamoto zinazowakabili ni sehemu ya kuishi wahudumu wa kituo hicho, mishahara ya kuwalipa wahudumu na makazi ya wahudumu wa kituo hicho.
Bi. Zuhuru Bakari alisema kituo hicho kinalea watoto 30 ambapo watoto 20 wanalelewa nje ya kituo kwa baadhi ya walezi waliowachagua wao kutokana na ufinyu wa eneo jumla yake inatengeneza idadi ya watoto 50.
Mwanafamilia Ester Ulaya akizungumza kwa niaba ya Jay Dee Family ambapo amesema watakuwa bega kwa bega na kituo hicho na kuendelea kuwatafutia wafadhili wa kusaidia kituo hicho.
Baadhi ya wanafamilia katika pozi na walezi wa kituo hicho.
Wanafamilia katika picha ya pamoja na walezi wa kituo hicho pamoja na watoto yatima wanaolelewa kwenye kituo hicho.
Zainul Mzige wa MO BLOG alijumuika na Familia ya Jay Dee katika kutoa msaada kwa watoto yatima wa kituo cha Maunga Centre.

SOURCE; LAY JAY DEE BLOG

0 comments: